MC MBUNI Cover Image
MC MBUNI Profile Picture
MC MBUNI
@mcmbuni3681224894 • 26 people like this
3 yrs - Translate

Ukosefu wa mvua kwa kipindi kirefu katika eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi umezua wasi wasi miongoni mwa wakazi huku wakihofia kukumbwa na baa la njaa.
Wakizungumza na mwanahabari wetu katika eneo hilo wenyeji hao wakiongozwa na David Bakari wamesema wameanza kushuhudia mabadiliko ya hali ya anga na hawana matumaini ya kushuhudia mvua na huenda baadhi yao wakapoteza maisha kufuatia makali ya njaa kwani tayari wale walioenda mijini kutafuta ajira wamelazimika kurudi mashinani baada ya janga la Korona kuathiri kazi zao.
Aidha sasa wanaitaka serikali ya kaunti ya Kilifi kuingilia kati na kuhakikisha kuwa wanapata mwafaka wa suala hilo kwa wakazi na taasisi za elimu zilizoko katika eneo hilo kwa kuanzisha mpango wa chakula kwa wanafunzi kama ilivyokuwa hapo awali.
Kwa upande wake msimamizi wa wadi ya Sokoke katika kaunti ndogo ya Ganze James Muye amethibitisha swala hilo huku akisema kuwa tayari serikali ya kuanti hii imechukua takwimu ili kuwawezesha kukabiliana na njaa kupitia idara ya Majanga kaunti ya Kilifi.

image
3 yrs - Translate

Washikadau katika sekta ya utalii kaunti ya Lamu wametaja mila na tamaduni za wenyeji kuchangia katika ongezeko la idadi ya watalii wanaozuru eneo hilo.
Akizungumza na wanahabari kisiwani Amu, Mohammed Wenje msimamizi wa makavazi kisiwani humo ametaja hatua ya watalii, kutaka kufahamu kwa kina aina ya vyakula na maisha ya wanajamii hao, ikiwemo jinsi wanavyoadhimisha sherehe zao hasa za kitamaduni.
Aidha ametoa wito kwa wakazi kulinda tamaduni zao kwani ni njia mojawapo, itakayochangia katika kuimarika kwa sekta ya utalii kisiwani humo na hata kaunti ya Lamu kwa jumla.

image
3 yrs - Translate

Hatimaye familia ya mchuna kahawa maeneo ya Tinderet ambaye aliaga mwaka wa 2014 itaweza kumzika marehemu baada ya mahakama ya Kisumu kusuluhisha mgogoro wa shamba.

Mwili wa Barack Ogada Ouko umekuwa katika chumba cha kuhifadhi maiti kwa miaka nane tangu mwezi wa Mei mwaka wa 2014.

Familia ya marehemu ilishindwa kumzika baada ya mzozo kuhusiana na shamba lao la uridhi lililo katika kijiji cha Tieng’re K’oranda kuanza walipoenda kumzika pale.

Inadaiwa kuwa Bwana James Onunga aliandamana na maafisa wa polisi kudai kuwa shamba lile lilikuwa lake na kupelekea kurudishwa kwa mwili wa Ogada kwenye chumba cha kuhif

image
3 yrs - Translate

Waakazi wa TanaRiver wana kila sababu ya kutabasamu baada ya serikali kutumia shilingi bilioni 1 katika miradi ya maji kaunti hiyo.

Akizungumza katika ziara yake kaunti hiyo, katibu katika wizara ya maji Joseph Irungu amesema kuwa wizara ya maji ina miradi mingi eneo la Tana River mojawapo ikiwa wa kuchimbwa kwa visima vya maji katika kila kijiji.

Aidha amesema kuwa atashirikiana na viongozi wa kaunti hiyo kuhakikisha uhaba wa maji unatatuliwa, kwani serikali inanuia kuchimba visima zaidi ya mia kaunti hiyo.

Irungu aidha ameongeza kuwa wizara ya maji pia itachimba mabwawa ya maji ili kuwasaidia wafugaji kuhifadhi maji wakti wa msimu wa mvua.

image
3 yrs - Translate

Wavuvi eneo la Watamu kaunti ya Kilifi wametakiwa na Mwenyekiti wa usimamizi wa bahari BMU eneo la Watamu Athman Mwambire kuchukua tahadhari wanapokuwa baharini.
Mwambire amesema bahari imekuwa ikichafuka mara kwa mara kutokana na mawimbi na upepo mkali ambao umekuwa ukishuhudiwa na kuhatarisha maisha na usalama wa wavuvi wanapoendeleza uvuvi wao kwenye bahari.
Akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu, amesema ipo haja ya wavuvi kujilinda na kuhakikisha usalama wao uko imara.
Aidha amewahimiza wavuvi ambao watavua kwa kipindi hiki kubeba vifaa vya kujisaidia endapo ajali itatokea na pia ametoa wito kwa serekali ya kauti na kitaifa kuwaletea vyombo zaidi vya uokozi ili ajali inapotokea msaada upatikane kwa haraka.

image
About

This page is going to be free to everyone interms of news content polities etc..

Install Palscity app